Psalms 139:1-6
Mungu Asiyeweza Kukwepwa
(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)
1 aEe Bwana, umenichunguza
na kunijua.
2 bUnajua ninapoketi na ninapoinuka;
unatambua mawazo yangu tokea mbali.
3 cUnafahamu kutoka kwangu na kulala kwangu;
unaelewa njia zangu zote.
4 dKabla neno halijafika katika ulimi wangu,
wewe walijua kikamilifu, Ee Bwana.
5 eUmenizunguka nyuma na mbele;
umeweka mkono wako juu yangu.
6 fMaarifa haya ni ya ajabu mno kwangu,
ni ya juu sana kwangu kuyafikia.
Copyright information for
SwhKC