Psalms 139:1-6

Mungu Asiyeweza Kukwepwa

(Kwa Mwimbishaji: Zaburi Ya Daudi)


1 aEe Bwana, umenichunguza
na kunijua.

2 bUnajua ninapoketi na ninapoinuka;
unatambua mawazo yangu tokea mbali.

3 cUnafahamu kutoka kwangu na kulala kwangu;
unaelewa njia zangu zote.

4 dKabla neno halijafika katika ulimi wangu,
wewe walijua kikamilifu, Ee Bwana.


5 eUmenizunguka nyuma na mbele;
umeweka mkono wako juu yangu.

6 fMaarifa haya ni ya ajabu mno kwangu,
ni ya juu sana kwangu kuyafikia.

Copyright information for SwhKC